Saturday, 2 November 2013

Afya

MAMBO 5 AMBAYO UNGEPENDA UFAHAMU KUHUSU AFYA YA MENO YAKO.

watu wengi huwa na hofu ya sintofahamu
hasa wanapofikiria kwenda kumwona
daktari wa meno. mambo 5 yafuatayo
yatakusaidia sana kufahamu nini utarajie
unapokwenda kufuata uchunguzi wa afya
ya kinywa na meno ama matibabu ya
magonjwa ya kinywa na meno.
1.uchunguzi wa afya ya kinywa na
meno hujuimuisha uchunguzi wa kansa
kinywani
unapokwenda kwa daktari wa kinywa na
meno kwa uchunguzi wa kawaida wa
kinywa na meno (dental check up visit),
kwa kawaida daktari wa kinywa na meno
hutazama hali ya kinywa na meno pia
huchunguza uwepo wa dalili za kansa
kinywani. inakadiriwa kuwa mtu mmoja
hufa kila saa la kutokana na ugonjwa wa
kansa kinywani huko marekani. ugonjwa
huu hatari unaoshambulia zaidi kuta za
kinywa, midomo-hasa mdomo wa chini-
pamoja na koo unatibika ikiwa
utatambuliwa mapema na kutibiwa
kikamilifu.
hivyo, kumwona daktari wa meno walau
mara mbili kwa mwaka (kila baada ya
miezi sita) na kuepuka matumizi ya
tumbaku/sigara vitakuwezesha kujikinga
na ugonjwa wa kansa ya kinywa na
madhara yake.
2. magonjwa ya fizi huathiri afya ya
mwili kwa ujumla
magonjwa ya fizi na meno ni chanzo kikuu
cha kupoteza meno kwa watu wenye umri
mkubwa/watu wazima, na pia magonjwa
haya huhusishwa na magonjwa ya moyo
na kiharusi (stroke).
ikiwa magonjwa haya ya fizi
yatatambuliwa mapema (gingivitis),
yanatibika vizuri na kuepusha madhara
zaidi.
ikiwa tatizo hili halitopata tiba mapema,
ugonjwa hukomaa zaidi (periodontitis)
ambapo mfupa unaoshikilia jino/meno
hushambuliwa na kuharibiwa.
kusafisha meno kwa kupiga mswaki mara
mbili kwa siku, matumizi ya nyuzi-safishi
(dental floss), kumwona daktari wa meno
kwa uchunguzi mara kwa mara na
kusafisha meno kitaalamu kwa tatibu wa
meno, kutasaidia kuepuka madhara ya
magonjwa ya fizi.
3. uchunguzi wa kinywa na kusafisha
meno kitaalamu ni tiba muhimu zaidi
ni wangapi kati yetu wenye desturi ya
kumwona daktari wa meno walau mara
mbili kwa mwaka (walau kila baada ya
miezi sita)? mara nyingi wengi wetu
huhangaika na foleni za kumwona daktari
wa meno pale tu tunaposumbuliwa na
maumivu ama ya jino ama kidonda
kinywani ama kwa sababi ya hali zinginezo
zinatotulazimisha kumwona daktari wa
meno.
kusubiri mpaka tusukumwe na maumivu
ya meno/kidonda kinywani ama ajali
yoyote kunatunyima fursa bora zaidi ya
kuchunguzwa afya ya kinywa na meno na
kusafishwa meno ili kuepusha madhara ya
magonjwa ya kinywa na meno kabla
hayajatokea ama kukomaa.
4.kupiga mswaki mara mbili kwa siku
kunaepusha kuoza kwa meno.
kupiga mswaki kwa ufanisi walau mara
mbili kwa siku huondoa ukoko
unaogandiana kinywani na kusababisha
kuoza kwa meno. ukoko huu ni ute laini
unaoganda kwenye sehemu mbalimbali za
jino/meno
huku ukiwa na mamilioni ya vimelea vya
magonjwa (bakteria). matumizi ya nyuzi-
safishi (dental floss) kila
siku husaidia kuondosha ukoko maeneo
ambako mswaki haufiki, vile vile
kuondosha ukoko huu kunasaidia
kujikinga na magonjwa ya fizi.
5. magonjwa ya kinywa na meno
husababisha harufu mbaya mdomoni
takribani asilimia 85 ya watu wenye
harufu mbaya kinywani huwa na
magonjwa ya kinywa na meno,ikiwa
harufu mbaya kinywani inasababishwa na
magonjwa kinywani, dawa za kusafisha
kinywa (mouthwash) haziwezi kuondoa
tatizo zaidi ya kulifunika kwa muda tu.
hakuna sababu ya kuona haya
kumwambia daktari wa meno kuhusu
harufu mbaya kinywani inayokusumbua,
kwa vile kumwambia na kujadili tatizo lako
ni njia ya kuelekea kwenye tiba ya uhakika.
matumizi ya nyuzi-
safishi (dental floss) kila siku, kusafisha
meno na ulimi kwa mswaki walau mara
mbili kwa siku yaweza kuondoa harufu
mbaya kinywani kwa kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment